Tuesday, September 10, 2024

CHUNYA KUTUMIA BIILIONI 3 UJENZI KITUO CHA MABASI

Zaidi ya Sh 3 bilioni zinatarajiwa kutekeleza mradi wa ujenzi wa kituo cha kisasa cha mabasi Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya chenye uwezo wa kuegesha  mabasi 100 kwa siku na vibanda 400 vya biashara.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chunya Bosco Mwangine amesema Septemba 9, 2024 wakati wa hafla ya utiaji saini ujenzi wa mradi huo baina ya Halmashauri na mkandarasi mshauri wa Kampuni ya Malk Consultants LTD ambayo itajenga kwa miezi tisa.

Mwangine amesema mradi huo utakuwa na miundombinu ya huduma mbalimbali zikiwepo za kifedha  sambamba na mabanda 400 ya biashara na kuchochea fursa kubwa kwa wananchi.

Monday, August 26, 2024

MEYA ISSA: DKT. TULIA MBUNGE MAKINI, MAHIRI KULETA MAENDELEO MBEYA

Mstahiki Meya Jiji la Mbeya Dourmohamed Issa, amesema umahili wa Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya mjini Dkt. Tulia Ackson ameleta mabadiliko makubwa kwa Jiji la Mbeya katika kuleta maendeleo ya miradi ya kimkakati.

Issa amesema mara baada ya kushiriki mbio za mwenge wa Uhuru kitaifa 2024 wakati wa kuweka jiwe la msingi kwenye  mradi wa Maji Itagano - Mwanswekwa wenye thamani ya Sh 5 bilioni wenye uwezo wa kuzalisha maji lita milioni mbili kwa siku.

Amesema Dkt. Tulia ni Mbunge wa kitofauti kwa mahiri na umakini na amekuwa anafikika namna ya kulipambania jimbo la Mbeya kuleta maendeleo ikiwepo utekelezaji wa mradi huo wa Maji ambao utakuwa na tija kubwa kwa wananchi.

FYANDOMO: DKT. SAMIA AMETATUA CHANGAMOTO ZA WANANCHI MBEYA

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya, Suma Fyandomo amesema kitendo cha Rais Samia Suluhu Hassan kuleta fedha za miradi ya Maendeleo amelenga kutatua kero za wananchi hususan katika sekta ya afya na Maji.

Fyandomo amesema leo Jijini Mbeya baada ya kushiriki mbio za Mwenye wa Uhuru Kitaifa 2024  akiwa   amewawakilisha Wabunge wa Mkoa wa Mbeya.

Amesema kikubwa wanaendelea kuishukuru serikali kupitia  Rais Samia Suluhu Hassan na Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya mjini Dkt. Tulia Ackson kuwasilisha kero za wananchi.

"Kama mwakilishi wa wabunge nishukuru serikali na viongozi wa mbio za mwenge kwa kuja kuweka mawe ya msingi kwenye miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Mbeya" amesema.

Amesema kama wabunge wataendelea kushirikiana na serikali hususan kwa wananchi wa Mkoa wa Mbeya kutatua kero za wananchi katika maeneo mbalimbali.

THRDC YATOA MAFUNZO KWA WAANDISHI WA HABARI

Baadhi ya Waandishi wa habari kutoka mikoa mbalimbali, (kushoto Frolian Godwin kutoka Mwanza, Kenneth Ngelesi Kutoka Mbeya na Ediga Rwenduru kutoka Geita) wakiwa katika picha ya pamoja baada kushiriki mafunzo ya jinsi ya kuripoti habari za uchaguzi iliyofanyika Jijini Dodoma kwa siku mbili chini ya uratibu wa mtandao wa watetezi wa haki za binadamu THRDC.


Friday, August 16, 2024

WALIOHITIMU ELIMU YA KIDATO CHA SITA KWA UFADHIRI WA DKT. TULIA NIGERIA WAWASILI NCHINI

Wanafunzi  watano waliokuwa wakisoma nchini Nigeria kwa ufadhiri wa Taasisi ya Tulia Trust chini ya Mkurugenzi wa Spika wa Bunge Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) wamewasili leo Ijumaa Agost 16 mwaka huu.

Mapokezi hayo yamefanyika katika Uwanja wa Ndege wa Songwe huku ndugu jamaa na viongozi mbalimbali walishiriki wakiongozwa na Meneja wa Taasisi ya Tulia Trust Jackline Boaz.

Akizungumza mara baada ya mapokezi hayo Jackline amesema vijana hao watano akiwepo wa kiume mmoja walikuwa wakiishi katika mazingira magumu na kwamba walipata ufadhiri kuanzia kidato cha kwanza mpaka sita katika moja ya shule nchini Nigeria.

MKANDARASI WA MRADI MTO KIWIRA ATAKIWA KUONGEZA KASI

 

Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri amemtaka mhandisi mshauri wa Kampuni ya  GKW Consult GmbH kuharakisha ujenzi wa usanifu wa chanzo cha Maji Mto Kiwira Wilaya ya Rungwe kabla ya msimu wa kifuku kuanza.

Mhandisi Mwajuma amesema leo Mkoa wa Mbeya katika ziara yake ya kikazi ya kukagua ujenzi wa chanzo cha Mto Kiwira na tenki la Maji katika eneo la New Forest.

Amesema mhandisi mshauri anapaswa kuongeza nguvu ya ujenzi ili kwenda na kasi mvua zikianza watashindwa kutekeleza na kukamilika ifikapo Aprili 2025 kama makubaliano ya mkataba ulivyosainiwa.

Wednesday, August 14, 2024

"JIJI WEKENI MFUMO MZURI WA BAJAJI KUSHUSHA ABIRIA STENDI KUU" MWASELELA

Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM Taifa (NEC) Mkoa wa Mbeya Ndele Mwaselela  ameutaka uongozi wa halmashauri ya Jiji kuweka mfumo mzuri wa ulipaji wa ushuru wa madereva bajaji na kuwaruhusu kushusha abiria stend kuu ya mabasi ya mikoani.

Mwaselela amesema leo Agosti 14 mwaka huu wakati akizungumza na waandishi wa habari ikiwa ni siku ya tatu tangu akutane na madereva wa bajaji jiji la Mbeya zaidi ya 2,000 kwa lengo la kusikiliza kero zao.

Amesema miongoni mwa kero alizopokea na kuzitolea majibu  ni pamoja na  bajaji kuzuiwa kuingia kushusha abiria ndani ya stendi kuu hali  hali ambayo inahatarisha usalama wa abiria .

"Kuna eneo ambalo wametengewa lakini wamelalamikia sio rafiki ambalo sambamba na sehemu za maegesho ambayo itakuwa na maelekezo ili waweze kulipia" amesema.

Tuesday, August 13, 2024

1,000 KUSHIRIKI MASHINDANO YA MAPISHI

 

Taasisi ya Tulia Trust chini ya Mkurugenzi Wake ambaye ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson imeandaa Mashindano ya Mapishi kwa Mama na Baba Lishe  Mbeya Mjini.

Mashindano hayo yanajulikana kama  Tulia Cooking Festival yanatarajiwa kufanyika mwishoni mwa Mwezi Agosti  2024 na  yakishirikisha washiriki 1,000 yenye kauli mbiu isemayo tumia nishati mbadala kuondoa uchafuzi wa mazingira.

Taasisi ya Tulia Trust imekuwa ikifanya matamasha mbalimbali kwa ajili ya kuwapa fursa mbalimbali watanzania ikiwa ni pamoja na kuwainua kiuchumi.


Monday, August 12, 2024

DKT. NCHIMBI AAGIZA VIONGOZI WA CHADEMA, WAANDISHI WA HABARI WAACHIWE HURU


Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi amemwagiza Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Daniel Sillo kuzungumza na waziri wake, Hamad Masauni, kuwaachia huru viongozi wa Chadema waliokamatwa na Polisi mkoani Mbeya.

Dkt. Nchimbi amesema hayo leo Agosti 12, 2024 kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Katoro iliyopo mkoani Geita anakoendelea na ziara yake katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Amesema alifanya jitihada za kuwatafuta viongozi wenzake wa vyama vingine vya siasa, ili wawe na mazungumzo kama vyama vya siasa, aliwasiliana na baadhi ya makatibu wakuu, hata hivyo alipata taarifa wengine wamekamatwa mkoani Mbeya.

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUANDIKA HABARI ZA KUISAIDIA JAMII

Waandishi wa Habari nchini wametakiwa kuandika habari zitakazosaidia kutatua kero za wananchi kwa kuwa habari hizo zitasaidia kurejesha imani ya wananchi kwa vyombo vya habari.

Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari nchini (UTPC) Keneth Simbaya, aliyasema hayo mwishoni mwa wiki iliyopita alipozungumza na waandishi wa habari wa Mkoa wa Mbeya alipokuwa kwenye ziara ya kikazi mkoani humo.

Simbaya alisema kwa miaka ya karibuni imani ya wananchi kwenye vyombo vya habari imeshuka kutokana na waandishi wa habari kuripoti habari ambazo hazina tija kwao.


WANANCHI RUIWA NA MAHONGOLE WAOMBA KUTENGENEZEWA DARAJA LILILOHARIBIWA NA MAFURIKO

Wananchi wa Kata za Ruiwa na Mahongole Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya wameiomba Serikali kuwajengea daraja jingine eneo la Msikitini linalounganisha Kata ya Ilongo, Ruiwa na Mahongole lililoharibiwa na mvua za elinino mapema mwaka huu.

Wakiongea kwa nyakati tofauti wananchi hao wamesema daraja hilo kwa sasa ni hatarishi kwa waendesha bodaboda ambao wametengeneza kiunganishi cha muda kwa kutumia mbao na kwa sasa halina uwezo wa kupitisha magari hivyo kufanya gharama kubwa za nauli.

Diwani wa Kata ya Ruiwa Kassim Mtale amesema kukatika kwa daraja hilo kumeongeza umbali wa kilometa tatu kutoka daraja hilo kufika Ilongo.

Friday, August 9, 2024

JIJI LAAGIZWA KUTOA HATI KWA WANANCHI WALIOKUMBWA NA MAPOROMOKO YA TOPE

Halmashauri ya Jiji la Mbeya imetakiwa kutoa hati miliki za viwanja kwa wathirika wa maporomoko ya tope la mlima Kawetere kata ya Itezi jijini hapa.

Kauli hiyo imetolewa leo Ijumaa Agosti 9 mwaka huu mara baada ya Dkt. Tulia kufanya mkutano na waathirika hao kutatua mgogoro wa kujenga katika eneo walilopewa  viwanja kwa ajili ya makazi.

Sambamba na hilo Mbunge huyo na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) pia amekabidhi kitita cha Sh. milioni 25 zilizotolewa na Mwenyekiti Taifa wa Umoja wa Wanawake UWT Mary Chatanda.

Amesema awali baada ya kutokea maporomoko ya tope kutoka mlima Kawetere serikali ilitoa  maelekezo ya wananchi hao kupewa viwanja na sio kulipia hati miliki.

DKT. TULIA AWATOA HOFU WAFANYABIASHARA WA SOKO LA IGAWILO

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, amewataka Wafanyabiashara wa Soko la Igawilo lilolopo Kata ya Igawilo Jijini Mbeya kuendelea kufanya shughuli zao kwa amani ili kujipatia vipato vyao.

Dkt. Tulia ameyasema hayo Agosti 8, 2024 wakati alipofanya ziara ya kuwatembelea Wafanyabiashara wa soko hilo kwa lengo la kusikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi ambapo miongoni mwa kero walizomtajia ni pamoja na ubovu wa miundombinu, tozo za Halmashauri pamoja na muingiliano baina ya Wafanyabiashara wa ndani na nje ya soko hilo ambapo amewahakikishia kuzitatua kwa kushirikiana na Serikali.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya, Mhe. John Nchimbi, amesema kuwa Serikali imeanza kuzifanyia kazi changamoto za Wafanyabiashara hao na itahakikisha inazitatua kwa haraka.