Monday, August 25, 2025
PATRIC MWALUNENGE ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA UBUNGE MBEYA MJINI
MWANDISHI WA HABARI KUCHUANA NA SPIKA TULIA, UBUNGE JIMBO LA UYOLE
Ipyana amesema hatua hiyo ni sehemu ya dhamira yake ya kuwatumikia wananchi wa Uyole kwa uadilifu, uwajibikaji na kusimamia maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Amesisitiza kuwa chama chake kimejipanga kutoa mbadala mpya wa kiuongozi unaolenga kuleta matumaini mapya kwa wananchi.
Tuesday, July 29, 2025
WALIOTEULIWA KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE MAJIMBO YA MKOA WA MBEYA
Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), CPA Amos Makalla leo Jumanne Julai 29, 2025 ametangaza majina ya walioteuliwa na CCM kwenda hatua inayofuata ya kura za maoni ya chama hicho.
Saturday, July 26, 2025
AJALI YAUA WANAFUNZI WATANO WAKIKIMBIA MCHAKAMCHAKA, CHUNYA MBEYA
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya ACP Wilbert Siwa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambapo wanafunzi watano wamefariki papo hapo na majeruhi tisa wamepokelewa Kituo cha Afya Chalangwa.
Siwa amesema mara baada ya tukio dereva wa basi hilo alitoroka na juhudi za kumtafuta zinaendelea ambapo ametoa wito kwa madereva kuwa waangalifu wawapo barabarani na chanzo kikitajwa ni mwendo kasi na uzembe wa dereva.
Thursday, July 17, 2025
TULIA TRUST YAREJESHA TABASAMU FAMILIA NYUMBA ILIYOTEKETEA MOTO
Nyumba hiyo iliteketea kutokana na janga la moto lililotokea hivi karibuni hali iliyosababisha kukosa mahala pa kuishi.
Ukarabati huo unatekelezwa na Taasisi ya Tulia Trust ambayo Mkurugenzi wake ni Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson na Rais wa Mabunge Duniani (IPU), kupitia mpango wa Tulia Trust mtaani kwetu.
Mpango huo umekuwa na tija ya kurejesha tabasamu kwa wananachi wa Jiji la Mbeya zikiwepo kaya zisizojiweza, yatima na wazee.
Thursday, July 10, 2025
MAHAKAMA YATUPILIA MBALI KESI YA MDUDE
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya imetupilia mbali maombi ya jinai namba 14538/2025 yaliyofunguliwa mei 17,2025 na Sije Mbughi mke wa Mpaluka Nyagali (Mdude) dhidi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Mkurugenzi wa mashitaka (DPP), Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya(RPC), Mkuu wa upelelezi Mkoa wa Mbeya (RCO) na askari Shaban Charo anayedaiwa kuwa ndiye aliyemchukua Mdude ambapo maombi yameanza kusikilizwa Juni 30, 2025 na kutolewa uamuzi Julai 9, 2025 na Jaji Said Kalunde.
Mleta maombi Sije Mbughi amewakilishwa na Wakili Bonifase Mwabukusi, Wakili Hekima Mwasipu na Wakili Solomon Kamunyu ambapo upande wa wajibu maombi umewakilishwa na Wakili Domick Mushi pamoja na Wakili Adalbert Zegge huku Sije akitaka mumewe kufikishwa mahakamani na kufungulia mashitaka kwa mujibu wa sheria.
Jaji Said Kalunde ameanza kutoa uamuzi majira ya saa 9:35 alasiri na kuhitimishwa saa 11:50 jioni awali Jaji Said Kalunde amesema upande wa mleta maombi akiwemo Sije Mbughi na Ezekiel Sheyo.
Monday, June 30, 2025
MASACHE ACHUKUA FOMU YA KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE WA JIMBO LA LUPA, CHUNYA
MWALUNENGE AREJESHA FOMU YA KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE MBEYA MJINI
Sunday, June 29, 2025
MHANDISI MARYPRISCA MAHUNDI ACHUKUA FOMU KUTETEA NAFASI YAKE
Mhandisi Maryprisca Mahundi amefika katika ofisi za UWT Mkoa wa Mbeya kuchukua fomu ya kugombea Ubunge Viti Maalum Mkoa wa Mbeya.
Mhandisi Maryprisca Mahundi amechukua fomu hiyo ili kutetea nafasi yake ambayo ameitumikia muhula mmoja wa miaka mitano (2020-2025).
MWANAHABARI AJITOSA KUMKABILI MEYA WA JIJI LA MBEYA
Mwandishi wa Habari, David Nyembe (kushoto), akikabidhiwa fomu ya kuomba ridhaa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Isanga kuchaguliwa kuwa mgombea udiwani wa Kata hiyo katika Uchaguzi Mkuu wa Mwezi Oktoba mwaka huu.
Nyembe amekabidhiwa fomu na Katibu wa CCM Kata hiyo Golden Ndolela leo Juni 29, 2025.
Hadi kufikia leo majira ya saa nne asubuhi jumla ya wagombea watatu tayari wamechukua fomu ya kuomba ridhaa ya chama hicho kuwania nafasi hiyo akiwemo aliyekuwa Meya wa Jiji la Mbeya Mh. Dormohamed Issa.
Friday, June 20, 2025
HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA YAPOKEA MSAADA WA VIFAA VYA MATIBABU YA MACHO KWA WATOTO
Ameongeza kuwa msaada huo ni matokeo ya ushirikiano wanaopatiwa hivyo amewataka watumiaji wa vifaa hivyo kuvihifadhi vizuri ili viendelee kufanya kazi kwa ubora.