Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini Oran M. Njeza, amezitembele na kutoa mkono wa pole kwa familia za watu 29 waliofariki na majeruhi wa ajali.
Ajali hiyo ilitokea Juni 7, 2025 katika mtelemko mkali wa mlima Iwambi Wilaya ya Mbeya, baada ya ya lori lilokuwa limebeba shehena za unga kugonga magari mawili yakiwepo ya abiria.
Katika ajali hiyo watu 28 walipoteza maisha papo hapo na wengine tisa kujeruhiwa na kukimbizwa katika Hosptali Teule ya Ifisi Wilaya ya Mbeya.
Wednesday, June 18, 2025
NJEZA ATEMBELEA WAFIWA AJALI ILIYOUA 29 MLIMA IWAMBI
Wednesday, June 11, 2025
DC MALISA AMKABIDHI MEYA JIJI LA MBEYA KITABU MPANGO MKAKATI MIAKA MITANO
Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Malisa amezindua mpango mkakati wa Dira ya miaka mitano ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya na kumkabidhi rasmi Meya Jiji la Mbeya Dour Mohamed Issa
Makabidhiano hayo yamefanyika leo Jumatano Juni 11, 2025 katika ukumbi wa mikutano wa mkapa jijini hapa, ikiwa ni uzinduzi wa mpango mkakati wa dira ya miaka mitano ya 2025/26 mpaka 2029/2039 kwa halmashauri ya Jiji la Mbeya.
Dira hiyo imebeba vipaumbele 29 ikiwepo masuala ya elimu, afya maboresho ya teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) ujenzi wa bandari ya nchi kavu, sekta ya afya na elimu na mengineyo mengi.
Malisa amepongeza wadau walio fanikisha Halmashauri ya Jiji kutekeleza mkakati, huku akitaka kuweka kipaumbele katika uboreshwaji miundombunu ya masoko ili wafanya biashara waweze kufanya kazi masaa 24.
Monday, May 5, 2025
DC MALISA: WANANCHI CHANGAMKIENI FURSA UJIO MADAKTARI BINGWA BOBEZI 36 MBEYA
Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Beno Malisa, amehamasisha wananchi kutumia fursa ya ujio wa Madaktari Bingwa Bobezi wa Dkt Samia kufanyiwa vipimo vya uchunguzi wa magonjwa.
Kambi ya madaktari bingwa bobezi imeanza leo Mei 5 mpaka Mei 9, 2025 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya (Mbeya RRH) kwa muda wa siku tano.
Amesema huduma hizo zitawanufaisha wananchi kutoka mikoa Nyanda za Juu Kusini ikiwepo Mbeya, Ruvuma Songwe, Songea Njombe.
Awali mkazi wa Njombe Vaileth Kwese,amesema kitendo cha serikali kuwafikishia huduma kimewapunguzia gharama za kusafiri umbali mrefu kufuata matibabu.
Friday, May 2, 2025
MADAKTARI BINGWA BOBEZI WA SAMIA KUWEKA KAMBI HOSPTALI YA RUFAA MKOA MBEYA
Madaktari bingwa bobezi wa Mama Samia wanatarajia kuweka kambi ya siku tano ya kufanya uchunguzi wa magonjwa mbalimbali katika Hosptali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya.
Kambi hiyo imeratibiwa na Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Hosptali ya Rufaa kanda ya nyanda za juu kusini katika mikoa ya Songwe, Njombe, Songwe na Mbeya .
Akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa Mei 2, 2025, Mganga mfawidhi wa Hosptali ya Rufaa Mkoa wa Mbeya Dkt. Abdallah Mmbaga amesema kambi hiyo itaanza Mei 5 mpaka 9 mwaka huu.
Amesema madaktari bingwa bobezi wa Mama Samia wametoka katika Hosptali ya Taifa Muhimbili (MOI), Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Taasisi ya Benjamin Mkapa na Hosptali ya Rufaa Kanda ya Mbeya.
Dkt. Mmbaga amesema lengo ni kutoa huduma za kibingwa na kikobezi kwa wananchi wa mikoa ya nyanda za Juu Kusini hususani kwa wale wenye changamoto za kiafya zinazohitaji huduma za kitaalam.
Wednesday, April 30, 2025
DC MBARALI AMALIZA MGOGORO WA WAKULIMA, WAFUGAJI NA MWEKEZAJI SHAMBA LA NARCO MWATENGA
Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya Kanali Maulid Sulumbu amesikiliza kero Kitongoji cha Manzega Kijiji cha Kilambo Kata ya Mwatenga kuhusiana na mgogoro wa wananchi na mwekezaji David Kaaya wa Kampuni ya O.C Industrial Holdings katika shamba la NARCO.
Akifungua mkutano Mwenyekiti wa Kijiji cha Kilambo Mwakani Chagu mbali ya kushukuru ujio wa Mkuu wa Wilaya huku akiwataka wananchi kuwa watulivu.
Diwani wa Kata ya Mwatenga Omary Sagutangu amesema mgogoro wa mwekezaji na wananchi umedumu kwa muda mrefu hivyo ujio wa Mkuu wa Wilaya utakuwa suluhisho kwani vikao vingi vimefanyika katika ngazi mbalimbali bila mafanikio.
Frank Sichalwe Katibu Tawala Wilaya ya Mbarali amesema ofisi yake ilipokea malalamiko kutoka kwa wananchi hivyo kutokana na uzito huo Mkuu wa Wilaya amefika kwa ajili ya kuwasililiza.
Saturday, April 26, 2025
JOWUTA, THRDC WALAANI WANAHABARI KUKAMATWA NA KUPIGWA
Chama cha Wafanyakazi katika Vyombo vya Habari Tanzania (JOWUTA) na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binaadamu nchini (THRDC) wamelaani kuanza kuibuka matukio ya waandishi wa habari na watangazaji kukamatwa na baadhi kupigwa na hata kuharibiwa vifaa vyao vya kazi na vyombo vya dola.
Kauli ya kulaani imetolewa leo Aprili 25 mwaka huu na Mwenyekiti wa JOWUTA Mussa Juma leo mkoani Mbeya, wakati wa mafunzo kwa wanahabari kuhusu uandishi wa habari za uchaguzi, ulinzi na usalama kazini.
Mafunzo hayo yamehusisha waandishi kutoka mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe, ambapo Juma amesema matukio ya kukamatwa, kupigwa na kuharibiwa vitendea kazi hayakubaliki katika nchi inayojinadi kuwa inazingatia misingi ya kidemokrasia.
Sunday, April 20, 2025
“KWENYE UCHAGUZI HUU TUWE WATU WA KUSAMEHEANA” ASKOFU PANGANI
.zip%20-%201.jpeg)
Wito huo ameutoa katika maadhimisho ya ibada ya Sikukuu ya Pasaka iliyofanyika katika kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi Ushirika wa Ibala ulipo Halmashauri ya Jiji la Mbeya.
Wednesday, April 9, 2025
"TUPO TAYARI KWA UCHAGUZI, ILA TUNATAKA MABADILIKO HAYA" CHAUMMA
Tanzania inatarajia kufanya Uchaguzi Mkuu, Oktoba 25 mwaka huu kuwapata madiwani, wabunge na Rais, huku Chama hicho kikitarajia kusimamisha wagombea katika nafasi zote.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa Aprili 7, 2025, Katibu Mwenezi wa Chama hicho Taifa, Ipyana Njiku amesema katika kikao cha Halmashauri kuu ya Chama hicho Februari 19, 2025 kiliazimia kushiriki uchaguzi huo katika nafasi zote na kutoa mwelekeo wa nchi kwa miaka mitano ijayo.
Thursday, March 20, 2025
ENG. MAHUNDI AANZA ZIARA KUKAGUA HUDUMA ZA MAWASILIANO MPAKA WA KASUMULU NA TUNDUMA
Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) amewasili katika ofisi za Mkoa wa Mbeya na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa huo, Dkt. Juma Homera, leo Machi 20, 2025.
Akimkaribisha Naibu Waziri Mahundi, Mkuu wa Mkoa, Dkt. Homera, ameipongeza wizara kwa kazi nzuri inayofanya katika kuboresha hali ya mawasiliano mkoani humo.
Dkt. Homera ameomba Wizara kuhakikisha maeneo ya Utalii yanakuwa na mawasiliano bora zaidi ili kuchochea Sekta ya Utalii, pamoja na kuendelea kuboresha huduma za mawasiliano katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo, ikiwemo Kyela.
Kwa upande wake, Mhandisi Mahundi amesema ziara yake inalenga kukagua upatikanaji wa huduma za mawasiliano katika maeneo ya mpakani ya Kasumulu uliopo Mkoa wa Mbeya na Tunduma, mkoani Songwe, ambapo wakazi wa maeneo hayo wamekuwa wakikumbana na changamoto ya kupokea taarifa kutoka mitandao ya nchi jirani badala ya Tanzania.