Monday, September 30, 2024

DKT. TULIA, MAMA LISHE KUHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI

Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson ameungana na Mama Lishe katika Kata ya Uyole Jijini Mbeya kwa ajili ya kuandaa chakula kwa kutumia nishati safi ya gesi.

Dkt. Tulia ameshiriki tukio hilo leo Jumatatu  Septemba 30, 2024 kwa kuingia sokoni kufanya mahitaji mbalimbali huku akieleza lengo ni kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan kuhamasisha matumizi ya nishafi safi.

"Leo nashirikiana na Mama lishe kuandaa chakula kwa kutumia nishati safi lengo ni kuona wanabadilika kwa kuachana na matumizi ya kuni na mkaa ili kulinda  mazingira na kutunza rasilimali za miti" amesema Dkt. Tulia.

Friday, September 27, 2024

TANZANIA INASHIRIKI KONGAMANO LA TANO LA KIMATAIFA LA MASHIRIKIANO KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya kupambana na rushwa nchini (Takukuru), Crispin Chalamila amesema Serikali ya Tanzania imekuwa ikipambana na Rushwa kwa kuimarisha mifumo ya sheria na ya kitaasisi ikiwemo kuanzishwa kwa Divisheni ya Mahakama Kuu inayoshughulikia masuala ya Rushwa na Uhujumu Uchumi.

Chalamila ameyasema hayo leo katika Jiji la Beijing China wakati akiwasilisha mada iliyojulikana kama ‘ANTI CORRUPTION AND INSTITUTIONAL LEGAL FRAME WORK IN TANZANIA’ kwa Wakuu wa Mamlaka za Kuzuia na Kupambana na Rushwa wanaoshiriki kwenye kongamano la 5 la Kimataifa linalohusu mapambano dhidi ya rushwa (‘The 5th Global Operational Network of Anti Corruption Law Enforcement Authorities – GlobE Network’).

Kongamano hilo ni mahususi kwa ajili ya Mamlaka za Kuzuia na Kupambana Rushwa Duniani kubadilishana uzoefu na utaalamu katika jukumu la kuzuia na kupambana na Rushwa.

Aidha kongamano hilo la siku tano, linahudhuriwa na Mamlaka 219 za Kuzuia na Kupambana na Rushwa kutoka nchi 121 Duniani ikiwemo Tanzania ambapo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa wanashiriki.

Wednesday, September 25, 2024

DC MALISA: WANANCHI WASHIRIKI KUPINGA UKATILI

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Beno Malisa amehamasisha jamii kushiriki kikamilifu katika kampani ya "Tuwalinde kabla hawaja haribikiwa" kukabiliana na matukio ya ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto mashuleni.

Malisa amesema leo mara baada ya kuzindua kampeni hiyo huku akisisitiza wazazi, walezi na jamii kutekeleza majukumu yao kuwalinda watoto ili kuwa katika mazingira salama.

"Wazazi, walezi tekelezeni majukumu yenu kulinda na kuwa karibu na watoto ili kubaini changamoto zinazowakabili na kuwasilisha katika vyombo vya dola" amesema.


Tuesday, September 24, 2024

NSOKOLO 'WAANDISHI WA HABARI WANAPASWA KUWA MABALOZI WA NCHI ZAO'

Rais wa muungano wa klabu za waandishi wa habari Tanzania UTPC Deogratius Nsokolo amesema waandishi wa Habari barani Afrika wanapashwa kuwa mabalozi wa Nchi zao na kubeba jukumu la kuelimisha Umma juu ya utekelezaji wa miradi na mipango ya Serikali katika Nchi zao.

Ameyasema hayo wakati timu ya waandishi wa Habari kutoka nchi 11 za Afrika walipotembelea Mji wa kiserikali unaonendelea kujengwa Jijini Cairo nchini Misri ambapo, waandishi wameshuhudia namna Serikali ya Misri ilivyopanga na kuanza kutekeleza Mradi mkubwa wa kuhamisha makao makuu kutoka katikati ya Jiji la Cairo kwenda pembezoni mwa Jiji eneo lililopewa jina la Cairo mpya (New Administrative Capital City - ACUD).

Nsokolo amesema waandishi wana jukumu la kuuleza Umma juu ya manufaa ya miradi mikubwa inayotekelezwa katika Nchi zao na kufuatilia utekelezaji wake wakati wote ili wananchi na Dunia ijue kinachoendelea.

Tuesday, September 10, 2024

CHUNYA KUTUMIA BIILIONI 3 UJENZI KITUO CHA MABASI

Zaidi ya Sh 3 bilioni zinatarajiwa kutekeleza mradi wa ujenzi wa kituo cha kisasa cha mabasi Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya chenye uwezo wa kuegesha  mabasi 100 kwa siku na vibanda 400 vya biashara.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chunya Bosco Mwangine amesema Septemba 9, 2024 wakati wa hafla ya utiaji saini ujenzi wa mradi huo baina ya Halmashauri na mkandarasi mshauri wa Kampuni ya Malk Consultants LTD ambayo itajenga kwa miezi tisa.

Mwangine amesema mradi huo utakuwa na miundombinu ya huduma mbalimbali zikiwepo za kifedha  sambamba na mabanda 400 ya biashara na kuchochea fursa kubwa kwa wananchi.