Tuesday, September 10, 2024

CHUNYA KUTUMIA BIILIONI 3 UJENZI KITUO CHA MABASI

Zaidi ya Sh 3 bilioni zinatarajiwa kutekeleza mradi wa ujenzi wa kituo cha kisasa cha mabasi Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya chenye uwezo wa kuegesha  mabasi 100 kwa siku na vibanda 400 vya biashara.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chunya Bosco Mwangine amesema Septemba 9, 2024 wakati wa hafla ya utiaji saini ujenzi wa mradi huo baina ya Halmashauri na mkandarasi mshauri wa Kampuni ya Malk Consultants LTD ambayo itajenga kwa miezi tisa.

Mwangine amesema mradi huo utakuwa na miundombinu ya huduma mbalimbali zikiwepo za kifedha  sambamba na mabanda 400 ya biashara na kuchochea fursa kubwa kwa wananchi.