Monday, March 15, 2021

MAMA SAMIA: CHAPENI KAZI, MSIBABAISHWE NA MANENO YA WALIO NJE YA NCHI

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amewataka watanzania kushikamana na kutobabaishwa na maneno yanayozungumzwa na watu walioko nje ya nchi akiwahikikishia nchi iko salama.

Alisema hayo leo alipokuwa akiweka jiwe la msingi ujenzi wa jengo la ghorofa moja la Halmashauri ya Wilaya ya Handeni vijijini linalojengwa mjini Mkata.

Samia alisema ni kawaida kwa binadamu kupata hitilafu katika mwili kama mafua na kuwataka  watanzania kushikamana na kuliombea Taifa.


"Hakuna wakati muhimu ambao watanzania wanatakiwa kushikamana na kuliombea Taifa kama wakati huu," alisema Suluhu.

"Niwahakikishie wananchi wenzangu Tanzania tupo salama, chapeni kazi ili kuleta maendeleo... msibabaishwe na maneno ya watu walioko nje ya nchi," alisema Samia ambaye ameanza ziara ya siku tano mkoani Tanga.

Alielekeza kufurahishwa kwake na mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Handeni Vijijini ambalo linatarajiwa kugharimu sh 5.3 bilioni.

No comments:

Post a Comment