Tuesday, July 29, 2025
WALIOTEULIWA KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE MAJIMBO YA MKOA WA MBEYA
Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), CPA Amos Makalla leo Jumanne Julai 29, 2025 ametangaza majina ya walioteuliwa na CCM kwenda hatua inayofuata ya kura za maoni ya chama hicho.
Saturday, July 26, 2025
AJALI YAUA WANAFUNZI WATANO WAKIKIMBIA MCHAKAMCHAKA, CHUNYA MBEYA
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya ACP Wilbert Siwa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambapo wanafunzi watano wamefariki papo hapo na majeruhi tisa wamepokelewa Kituo cha Afya Chalangwa.
Siwa amesema mara baada ya tukio dereva wa basi hilo alitoroka na juhudi za kumtafuta zinaendelea ambapo ametoa wito kwa madereva kuwa waangalifu wawapo barabarani na chanzo kikitajwa ni mwendo kasi na uzembe wa dereva.
Thursday, July 17, 2025
TULIA TRUST YAREJESHA TABASAMU FAMILIA NYUMBA ILIYOTEKETEA MOTO
Nyumba hiyo iliteketea kutokana na janga la moto lililotokea hivi karibuni hali iliyosababisha kukosa mahala pa kuishi.
Ukarabati huo unatekelezwa na Taasisi ya Tulia Trust ambayo Mkurugenzi wake ni Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson na Rais wa Mabunge Duniani (IPU), kupitia mpango wa Tulia Trust mtaani kwetu.
Mpango huo umekuwa na tija ya kurejesha tabasamu kwa wananachi wa Jiji la Mbeya zikiwepo kaya zisizojiweza, yatima na wazee.
Thursday, July 10, 2025
MAHAKAMA YATUPILIA MBALI KESI YA MDUDE
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya imetupilia mbali maombi ya jinai namba 14538/2025 yaliyofunguliwa mei 17,2025 na Sije Mbughi mke wa Mpaluka Nyagali (Mdude) dhidi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Mkurugenzi wa mashitaka (DPP), Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya(RPC), Mkuu wa upelelezi Mkoa wa Mbeya (RCO) na askari Shaban Charo anayedaiwa kuwa ndiye aliyemchukua Mdude ambapo maombi yameanza kusikilizwa Juni 30, 2025 na kutolewa uamuzi Julai 9, 2025 na Jaji Said Kalunde.
Mleta maombi Sije Mbughi amewakilishwa na Wakili Bonifase Mwabukusi, Wakili Hekima Mwasipu na Wakili Solomon Kamunyu ambapo upande wa wajibu maombi umewakilishwa na Wakili Domick Mushi pamoja na Wakili Adalbert Zegge huku Sije akitaka mumewe kufikishwa mahakamani na kufungulia mashitaka kwa mujibu wa sheria.
Jaji Said Kalunde ameanza kutoa uamuzi majira ya saa 9:35 alasiri na kuhitimishwa saa 11:50 jioni awali Jaji Said Kalunde amesema upande wa mleta maombi akiwemo Sije Mbughi na Ezekiel Sheyo.