Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya Kanali Maulid Sulumbu amesikiliza kero Kitongoji cha Manzega Kijiji cha Kilambo Kata ya Mwatenga kuhusiana na mgogoro wa wananchi na mwekezaji David Kaaya wa Kampuni ya O.C Industrial Holdings katika shamba la NARCO.
Akifungua mkutano Mwenyekiti wa Kijiji cha Kilambo Mwakani Chagu mbali ya kushukuru ujio wa Mkuu wa Wilaya huku akiwataka wananchi kuwa watulivu.
Diwani wa Kata ya Mwatenga Omary Sagutangu amesema mgogoro wa mwekezaji na wananchi umedumu kwa muda mrefu hivyo ujio wa Mkuu wa Wilaya utakuwa suluhisho kwani vikao vingi vimefanyika katika ngazi mbalimbali bila mafanikio.
Frank Sichalwe Katibu Tawala Wilaya ya Mbarali amesema ofisi yake ilipokea malalamiko kutoka kwa wananchi hivyo kutokana na uzito huo Mkuu wa Wilaya amefika kwa ajili ya kuwasililiza.