Wednesday, April 30, 2025

DC MBARALI AMALIZA MGOGORO WA WAKULIMA, WAFUGAJI NA MWEKEZAJI SHAMBA LA NARCO MWATENGA


Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya Kanali Maulid Sulumbu amesikiliza kero Kitongoji cha Manzega Kijiji cha Kilambo Kata ya Mwatenga kuhusiana na mgogoro wa wananchi na mwekezaji David Kaaya wa Kampuni ya O.C Industrial Holdings katika shamba la NARCO.

Akifungua mkutano Mwenyekiti wa Kijiji cha Kilambo Mwakani Chagu mbali ya kushukuru ujio wa Mkuu wa Wilaya huku akiwataka wananchi kuwa watulivu.

Diwani wa Kata ya Mwatenga Omary Sagutangu amesema mgogoro wa mwekezaji na wananchi umedumu kwa muda mrefu hivyo ujio wa Mkuu wa Wilaya utakuwa suluhisho kwani vikao vingi vimefanyika katika ngazi mbalimbali bila mafanikio.

Frank Sichalwe Katibu Tawala Wilaya ya Mbarali amesema ofisi yake ilipokea malalamiko kutoka kwa wananchi hivyo kutokana na uzito huo Mkuu wa Wilaya amefika kwa ajili ya kuwasililiza.

Saturday, April 26, 2025

JOWUTA, THRDC WALAANI WANAHABARI KUKAMATWA NA KUPIGWA


Chama cha Wafanyakazi katika Vyombo vya Habari Tanzania (JOWUTA) na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binaadamu nchini (THRDC) wamelaani kuanza kuibuka matukio ya waandishi wa habari na watangazaji kukamatwa na baadhi kupigwa na hata kuharibiwa vifaa vyao vya kazi na vyombo vya dola.

Kauli ya kulaani imetolewa leo Aprili 25 mwaka huu na Mwenyekiti wa JOWUTA Mussa Juma leo mkoani Mbeya, wakati wa mafunzo kwa wanahabari kuhusu uandishi wa habari za uchaguzi, ulinzi na usalama kazini.

Mafunzo hayo yamehusisha waandishi kutoka mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe, ambapo Juma amesema matukio ya kukamatwa, kupigwa na kuharibiwa vitendea kazi hayakubaliki katika nchi inayojinadi kuwa inazingatia misingi ya kidemokrasia.

Sunday, April 20, 2025

“KWENYE UCHAGUZI HUU TUWE WATU WA KUSAMEHEANA” ASKOFU PANGANI ‎

Katika kuadhimisha Sikukuu ya Pasaka, Askofu wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi Robert Pangani amewataka waumini, viongozi wa serikali na dini kuwa na moyo wa msamaha kama ambavyo Mungu alivyousamehe ulimwengu kupitia Yesu Kristo aliyekufa na kufufuka kwa ajili ya mwanadamu.

‎Wito huo ameutoa katika maadhimisho ya ibada ya Sikukuu ya Pasaka iliyofanyika katika kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi Ushirika wa Ibala ulipo Halmashauri ya Jiji la Mbeya. 

Askofu Pangani amesema ili kuwa Mkristo   unayemwamini Mungu unapaswa kuwa na roho ya msamaha kwa kila mtu pasipo kujali kosa ulilofanyiwa.
‎Katika hatua nyingine amewataka watanzania kuendelea kuitunza amani ya nchi huku akiwataka wanasiasa kutokuwa na lugha za kuleta migogoro kwenye jamii kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu October, 2025 huku akisema utunzwaji wa amani unaanzia kwenye familia.
‎Kwa upande wake mchungaji wa ushirika wa Ibala Kanisa la Moravian Alinuwila Swillah amesema kila mtanzania anawajibu wa kulinda amani huku waumini walioshiriki ibada hiyo ya Pasaka wakisema viongozi wa dini wanapaswa kuwa mstari wa mbele kukemea uovu unatendeka kwenye jamii.

Wednesday, April 9, 2025

"TUPO TAYARI KWA UCHAGUZI, ILA TUNATAKA MABADILIKO HAYA" CHAUMMA

Pamoja na kuthibitisha kushiriki Uchaguzi Mkuu mwaka huu, Chama Cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) kimependekeza na kuishauri Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi baadhi ya mambo kufanyiwa marekebisho kabla ya zoezi hilo.

Tanzania inatarajia kufanya Uchaguzi Mkuu, Oktoba 25 mwaka huu kuwapata madiwani, wabunge na Rais, huku Chama hicho kikitarajia kusimamisha wagombea katika nafasi zote.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa Aprili 7, 2025, Katibu Mwenezi wa Chama hicho Taifa, Ipyana Njiku amesema katika kikao cha Halmashauri kuu ya Chama hicho Februari 19, 2025 kiliazimia kushiriki uchaguzi huo katika nafasi zote na kutoa mwelekeo wa nchi kwa miaka mitano ijayo.