Thursday, November 30, 2023

HALMASHAURI YA WILAYA YA RUNGWE KUJENGA MAEGESHO YA BODABODA


Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Renatus Mchau ameahidi kujenga vituo vya maegesho ya bodaboda katika mji wa Tukuyu na vitongoji vyake ikiwa ni jitihada ya kuboresha mazingira ya usafirishaji wa abiria na mali zao.

Ahadi hii ameitoa katika kikao maalumu cha viongozi wa Bodaboda ambapo pamoja na viongozi wengine pia Kikosi cha Usalama Barabarani kutoka jeshi la polisi kimeshiriki.

Thursday, November 16, 2023

WAWEKAZAJI WA UTALII MKOA WA TANGA WATAKIWA KUJIANDAA NA MKUTANO WA WADAU WA MAZAO YA NYUKI DUNIANI 2027.

Wadau wa sekta ya utalii, sekta ya ufugaji nyuki na mazao yatokanayo na Nyuki wametakiwa kujiandaa na mkutano mkubwa wa wadau wa ufugaji nyuki na wazalishaji wa mazao yatokanayo na ufugaji nyuki utakao fanyika Jijiji Arusha mwaka 2027.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dunstan Kitandula amesema hayo alipokuwa anatoa salamu za Wizara kwenye Kongamano la Uwekezaji, Biashara na Utalii na Uzinduzi wa Mwongozo wa uwekezaji Mkoa wa Tanga.

Mh. Kitandula alisema kwamba kupitia mada mbalimbali zitakazowasilishwa katika kongamano na maonesho yanayoendelea katika mabanda, anaamini kuwa wawekezaji wengi watavutiwa kuja kuwekeza katika Mkoa wa Tanga kwani fursa nyingi zitaelezwa hapa zikiwemo za sekta ya Utalii.