Monday, November 1, 2021

MAADHIMISHO YA WIKI YA MSAADA WA SHERIA 2021 KUFANYIKA KITAIFA MKOANI MBEYA

Mh. Juma Homera, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.

 Na Keneth Mwakandyali.

Wananchi mkoani wa Mbeya wametakiwa kujitokeza kwa wingi kutumia fursa ya Maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Sheria inayofanyika kitaifa mkoani hapa kuanzia Novemba 01 hadi Novemba 12 katika viwanja vya Ruanda Nzovwe.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera leo Novemba alipokua akitoa akizungumza na waandishi wa Habari ambapo amewataka wananchi kuchangamkia fursa hii ili kuweza kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.

“Kutakuwa na timu ya wataalamu watakaokua wanazunguka maeneo mbalimbali ya wazi, vizuizini, mashuleni kutoa elimu wa msaada wa kisheria katika Nyanja tofauti kama ardhi, ndoa, mirathi, haki za wanawake, watoto na watu wenye ulemavu kuanzia Novemba 01 mpaka Novemba 07”
 
“Kuna changamoto nyingi kwenye secta hii ndio maana shughuli hii ya wiki wa msaada wa kisheria kufanyika kitaifa mkoani Mbeya inakwenda kuleta fursa kwa wananchi wenye changamoto mbalimbali kuweza kujua haki zao” alisema Homera
 
Naye mratibu wa Chama cha Sheria Tanganyika Kanda ya Mbeya Gerinus Mzanila amewahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi kupata fursa ya kuweza kusaidiwa changamoto za kisheria walizonazo na kujitanua katika nyanja za kisheria.
 
“huduma ya msaada wa kisheria ni huduma ambayo inatolewa kwa mtu ambae hana uwezo wa kumudu gharama za huduma ya kisheria, zile ambazo zinatolewa mahakamani au kwa wakili. Huduma ya kisheria ipo katika nyanja nyingi kama vile kumuhoji na kusikiliza jambo lake, kumsaidia kuandaa nyaraka anazotakiwa kwenda kuzisajili mahakamani, usuluhishi wa amani, pia kutoa elimu kuhusiana na mambo mbalimbali ya kisheria” amesema Mzanila 
 
Aidha Afisa Maendeleo ya Jamii  Mkoa wa Mbeya Stella Kategile ameeleza kuwa wiki ya msaada wa kisheria imekua msaada mkubwa katika jamii kwani imejikita zaidi katika kutoa msaada kwa wananchi ambao hawana kipato na kushindwa kumudu gharama za huduma ya kisheria.

No comments:

Post a Comment