Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji amewaasa watalaam wa utoaji salama wa dawa za usingizi katika shule ya dawa za usingizi iliyopo Hospitali ya Rufaa ya Kanda hiyo kuwa wanaporudi kwenye vituo vyao vya kazi kuendeleza ujuzi, elimu waliyopata pamoja na ushirikiano walioupata ili kuboresha huduma za upasuaji nchini.
Aidha Mkurugenzi huyo amewataka watalaam hao kujikita katika mbinu nyingine ya kujiongezea kipato ili kustawisha uchumi wao binafsi.