Wednesday, March 17, 2021

WATAALAMU WA DAWA ZA USINGIZI WAASWA KUENDELEZA UJUZI WA ELIMU WALIYOPATA

 Na Esther Macha.
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji  amewaasa watalaam wa utoaji salama wa  dawa za usingizi katika shule ya dawa za usingizi iliyopo Hospitali ya Rufaa ya Kanda hiyo kuwa wanaporudi kwenye vituo vyao vya kazi kuendeleza ujuzi, elimu waliyopata pamoja na ushirikiano walioupata ili kuboresha huduma za upasuaji nchini.

Aidha Mkurugenzi huyo amewataka watalaam hao kujikita katika mbinu nyingine ya kujiongezea kipato ili kustawisha uchumi wao binafsi.
 Dkt . Mbwanji alisema hayo jana wakati wa wa mahafali ya kwanza ya mafunzo ya utoaji dawa za usingizi kwa wahitimu 36 mafunzo ambayo yamefanyika kwa muda wa mwaka mmoja katika hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Mbeya

Monday, March 15, 2021

MAMA SAMIA: CHAPENI KAZI, MSIBABAISHWE NA MANENO YA WALIO NJE YA NCHI

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amewataka watanzania kushikamana na kutobabaishwa na maneno yanayozungumzwa na watu walioko nje ya nchi akiwahikikishia nchi iko salama.

Alisema hayo leo alipokuwa akiweka jiwe la msingi ujenzi wa jengo la ghorofa moja la Halmashauri ya Wilaya ya Handeni vijijini linalojengwa mjini Mkata.

Samia alisema ni kawaida kwa binadamu kupata hitilafu katika mwili kama mafua na kuwataka  watanzania kushikamana na kuliombea Taifa.


"Hakuna wakati muhimu ambao watanzania wanatakiwa kushikamana na kuliombea Taifa kama wakati huu," alisema Suluhu.

"Niwahakikishie wananchi wenzangu Tanzania tupo salama, chapeni kazi ili kuleta maendeleo... msibabaishwe na maneno ya watu walioko nje ya nchi," alisema Samia ambaye ameanza ziara ya siku tano mkoani Tanga.

Alielekeza kufurahishwa kwake na mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Handeni Vijijini ambalo linatarajiwa kugharimu sh 5.3 bilioni.