Monday, May 5, 2025

DC MALISA: WANANCHI CHANGAMKIENI FURSA UJIO MADAKTARI BINGWA BOBEZI 36 MBEYA

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Beno Malisa, amehamasisha wananchi kutumia fursa ya ujio wa Madaktari Bingwa  Bobezi wa Dkt Samia  kufanyiwa vipimo vya uchunguzi wa magonjwa.

Kambi ya madaktari bingwa bobezi imeanza leo Mei 5 mpaka  Mei 9, 2025 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya (Mbeya RRH) kwa  muda wa siku tano.

Amesema huduma hizo zitawanufaisha wananchi kutoka mikoa Nyanda za Juu Kusini  ikiwepo  Mbeya, Ruvuma Songwe, Songea  Njombe.

Awali mkazi wa Njombe Vaileth Kwese,amesema kitendo cha serikali kuwafikishia huduma kimewapunguzia gharama za kusafiri umbali mrefu kufuata matibabu.

Friday, May 2, 2025

JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA LAKANUSHA KUMKAMATA MDUDE

MADAKTARI BINGWA BOBEZI WA SAMIA KUWEKA KAMBI HOSPTALI YA RUFAA MKOA MBEYA

Madaktari bingwa bobezi wa Mama Samia wanatarajia kuweka kambi ya siku tano ya kufanya uchunguzi wa magonjwa mbalimbali katika Hosptali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya.

Kambi hiyo imeratibiwa na Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Hosptali ya Rufaa kanda ya nyanda za juu kusini katika mikoa ya Songwe, Njombe, Songwe na Mbeya .

Akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa Mei 2, 2025, Mganga mfawidhi wa Hosptali ya Rufaa Mkoa wa Mbeya Dkt. Abdallah Mmbaga amesema kambi hiyo itaanza Mei 5 mpaka 9 mwaka huu.

Amesema  madaktari bingwa bobezi wa Mama Samia wametoka katika Hosptali ya Taifa Muhimbili (MOI), Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Taasisi ya  Benjamin Mkapa na Hosptali ya Rufaa Kanda ya Mbeya.


Dkt. Mmbaga amesema lengo ni kutoa huduma za kibingwa na kikobezi kwa wananchi wa mikoa ya nyanda za Juu Kusini hususani kwa wale wenye changamoto za kiafya zinazohitaji huduma za kitaalam.