Saturday, August 21, 2021

TANLAP YAWANOA WANAHABARI MBEYA


 Na Hannelore Mrosso,

Mtandao wa watoa msaada wa sheria Tanzania (TANLAP) umeendesha mafunzo ya siku moja kwa waandishi wa habari mkoani Mbeya ili kuwaongezea uelewa juu ya umuhimu wa kuzingatia sheria inayosimamia utoaji wa huduma ya habari katika utendaji kazi wao wa kila siku.

Mafunzo hayo yamefanyika Agosti 20 mwaka huu yakihusisha watendaji mbalimbali kutoka taasisi isiyo ya kiserikali inayotoa msaada wa kisheria ijulikanayo kama SAUTI YA HAKI.

Kaimu mkurugenzi mtendaji wa TANLAP Bw. Machereli Machumbana amewaambia waandishi wa habari kuwa mtandao huo ulianzishwa mwaka 2006 na kusajiliwa mwaka 2009 ambapo mpaka sasa una wanachama 76, unalenga kuwakumbusha wanahabari kuhusu sheria mbalimbali zinazoongoza na kusimamia tasnia ya habari ili kuepuka kukinzana na sheria hizo hatimaye kujikuta wanakumbana na makosa ya kisheria.