Sunday, October 12, 2025

MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA UYOLE AFANYA KAMPENI MGUU KWA MGUU

 

Mgombea ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Ipyana Samson Njiku, ameendelea na kampeni zake za mguu kwa mguu kwa wananchi wa Jimbo la Uyole, ambapo leo ametembelea maeneo ya Kata ya Itezi na Igawilo akiwahamasisha wananchi kujiandaa kwa mabadiliko chanya kupitia uongozi makini na wenye dira ya maendeleo.

Akizungumza na wananchi katika maeneo mbalimbali , Njiku amesema kuwa endapo atapata ridhaa ya wananchi wa Uyole, ataweka kipaumbele katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo:

Ujenzi wa Soko la Kisasa na Kimataifa litakalowezesha wakulima na wafanyabiashara kuuza mazao yao ndani na nje ya nchi kwa urahisi, kuongeza ajira na kipato cha wananchi.